Habari

Bulaya kumburuza mahakamani Stephen Wasira

Mkutano wa kwanza wa Mbunge wa jimbo la Bunda Mjini Ester Bulaya baada ya kukamilika kwa kesi iliyokuwa ikimkabili mahakamani dhidi ya Stephen Wasira aliyekuwa mgombea kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ambaye alipinga matokeo ya Mbunge huyo anaenda kufungua kesi ya madai ya fidia.

Katika mkutano wake huo wananchi mbalimbali wa Bunda mkoani Mara wakati wananchi wakiwa na kiu ya kutaka kujua Bulaya kama atamsamehe Wasira au atamdai fidia.

“Tukitoka hapa tunaenda kufungua fidia kudai madai yetu tulete maendeleo Bunda sawasawa nimetenga milioni 20 kata 7 zote za mjini tuendelee kusambambaza mabomba ya maji ili kuondoa shida ya maji, mimi sifanyi kazi kwa maneno nafanya kazi kwa vitendo,” alisema Bulaya.

Hata hivyo wananchi wa Bunda wamemtaka mbyunge wao kudai fidia dhidi ya kesi iliyokua inamkabili kufuatia mbune Steven Wasira kufungua kesi na kusema kuwa ushindi wa Bulaya haukua halali.

Na Emmy Mwaipopo

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents