Habari
Bunge laahirishwa hadi mwakani
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, amehairisha vikao vya Bunge la 11 mkutano wa 9 leo Mjini Dodoma hadi tarehe 30, mwezi wa 1 mwaka 2018 siku ya Jumanne.
Waziri Majaliwa amehairisha vikao hivyo wakati akitoa hoja za Kuhairishwa kwa Bunge Mjini humo.
“Mhe. Spika baada ya kusema hayo naomba kutoa haja kuwa bunge lako tukufu sasa lihairishwe hadi tarehe 30 siku ya Jumanne mwezi wa 1 mwaka 2018. Mhe. Spika naomba kutoa hoja,” amesema Waziri Mkuu.