Habari
Bunge lahairishwa hadi Novemba
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, amehairisha vikao vya bunge leo Mjini Dodoma hadi tarehe 7, mwezi wa 11 saa 3:00 asubuhi siku ya Jumanne.
Waziri Majaliwa ameyazungumza hayo wakati akitoa hoja za Kuhairishwa kwa bunge Mjini humo.
“Mhe. Spika baada ya kusema hayo naomba kutoa haja kuwa bunge lako tukufu sasa lihairishwe hadi tarehe 7 siku ya Jumanne mwezi wa 11 mwaka 2017 tutakapo kutana tena hapa saa 3 asubuhi hapa Mjini Dodoma. Mhe. Spika naomba kutoa hoja,” amesema Waziri Mkuu.