Habari

Bunge lapitisha Muswada wa Sheria ya Huduma za Habari wa mwaka 2016

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limeupitisha Muswada wa Sheria ya Huduma za Habari wa mwaka 2016 uliojadiliwa kwa siku mbili.
14925281_10154693236099339_5016656658260990178_n
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye (katikati) akiwa mwenye furaha

Mswada huo uliwasilishwa bungeni jana mjini Dodoma na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye kisha wabunge wakaanza kuujadili.

Ukurasa wa twitter wa Msemaji Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, umetoa taarifa hii:

Bunge limepitisha Muswada wa Sheria ya Huduma za Habari, 2016.Muswada huo sasa unasubiri kusainiwa na Rais kuwa sheria kamili.

Mapema jana wakati wamajadiliano mbunge wa Kondoa ambaye alikuwa Waziri wa Habari katika serikali iliyopita, Mhe.Juma Nkamia alisema muswada huyo ukipitishwa na kuwa sheria utamaliza matatizo na kujenga heshima kwa waandishi wa habari.

Hata hivyo wabunge wa upinzani waliupinga muswada huyo kwa madai umempatia mamlaka makubwa waziri.

Picha chanzo Mwananchi

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents