Bushoke kurudisha tuzo ya watu
Kali ambayo imejiri katka kinyang’anyiro cha Kilimanjaro Music Awards ni baada ya msanii wa muziki wa kizazi kipya almaarif kwa jina la bushoke kutunikiwa tuzo ambayo sio ya kwake na kudai kuwa anahitaji kuirudisha,
Kali ambayo imejiri katka kinyang’anyiro cha Kilimanjaro Music Awards ni baada ya msanii wa muziki wa kizazi kipya almaarif kwa jina la bushoke kutunikiwa tuzo ambayo sio ya kwake na kudai kuwa anahitaji kuirudisha, hali ambayo inaashiria kuna makosa ambayo yamejitokeza katika uelewa wa haraka haraka kwa waandaaji.
Hii ni baada ya msanii Bushoke kutunukiwa tuzo ya wimbo bora wa zouk lakini wimbo uliotajwa ni wa msanii kutoka nchi Uganda ajulikanaye kwa jina la Juliana Kanyumuzi ambaye amemshirikisha Bushoke na sio wa Bushoke kama ilivyotangazwa hivyo tuzo imekwenda sipo.
Wimbo huo uliopo katika mahadhi ya zouk na unajulikana kwa jina ‘Mbali Nami’ na ndani yake zinasikika sauti mbili ikiwa ni ya Juliana ambayo inakuwa na kama inauongoza wimbo halikadhalika ya Bushoke.
Kauli kutoka kwa waandaaji inatakiwa isikike kuhusiana na siala hili kwani, hali kama hii inaweza kusababisha matatizo baina ya Bushoke na Juliana kwa kile kinachodhaniwa kuwa Bushoke katumia wimbo wa watu kuchukulia tuzo, hivyo ni muhimu hili lifanyiwe kazi, iwapo Bushoke atarud