Habari
Bwana Misosi afiwa na kaka yake anayemfuata
Rapper wa Tanga Joseph Rushahu aka Bwana Misosi amefiwa na kaka yake anayemfuata asubuhi ya leo. Katika ujumbe aliotutumia, Misosi amesema, “Kaka yangu mimi toka nitoke Emmanuel Rushahu kafariki leo mida ya saa 3 asubuhi hapa Muhimbili. Mungu kampenda zaidi, Amen.”
Bongo5 inampa pole Bwana Misosi kwa msiba huo wa kaka yake.