Muziki

CAF: Kikosi cha wachezaji wa Serengeti Boys U-17, Gabon yatajwa

CAF, yataja vikosi vinane vitakavyoshiriki michuano ya 12 Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa vijana chini ya umri wa miaka 17 nchini Gabon 2017.
Michuano hiyo mikubwa kabisa kwa Afrika inatarajiwa kuanza Mei 14 hadi 28 mwaka huu katika miji ya Libreville na Franceville nchini na kila timu itakuwa na wachezaji 21 kikosini.

Timu nane zimegawanywa katika makundi mawili, A likiundwa na wenyeji Gabon, Guinea, Cameroon na Ghana na B likiundwa na Mali, Tanzania, Angola na Niger. Timu mbili za juu katika kila kundi zitafuzu moja kwa moja Fainali za Kombe la Dunia, ambazo zitafanyika nchini India kuanzia Oktoba 6 hadi 28, mwaka huu.

BY HAMZA FUMO

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents