Michezo
CAF yabadili waamuzi kwenye mchezo wa TP Mazembe dhidi ya Simba
Shirikisho la soka barani Afrika CAF limefanya mabadiliko ya waamuzi watakao chezesha mchezo wa marudiano kati ya TP Mazembe dhidi ya Simba ambao utachezwa katika mji wa Lubumbashi nchini DR Congo.
Caf wamefanya mabadiliko hayo kwa kuwabadili waamuzi kutoka Ethiopia, na Kenya kwa kuwaweka waamuzi kutoka Zambia, sababu hasa zilizoelezwa za kuwabadili waamuzi hao ni pamoja na baadhi ya malalamiko yaliyotolewa na timu ya TP Mazembe kuwa kuna hujuma zilitolewa ambazo walidai wamefanyiwa hujuma na Simba.
By Ally Juma.