Burudani
Camp Mulla na Octopizzo waitaka midundo ya Pancho Latino
Kundi la Hip Hop la Kenya la Camp Mulla na hitmaker wa Ivo Ivo Octopizzo hivi karibuni watasikika kwenye midundo ya mpishi kijana wa B’Hits, Pancho Latino.
“Yap ni kweli natarajia kufanya nao kazi za muziki kwani kwa sasa ndio tupo katika michakato ya mazungumzo kwa hiyo napenda kuwambia wale mashabiki wangu wakae tayari kwa kusikia kile ambacho nitakacho wafanyia Camp mulla na Octopizzo,” Dj Fetty alimnukuu producer huyo.
Hivi karibuni Camp Mulla waliachia ngoma yao mpya waliomshirikisha msanii wa Nigeria, Wizkid.