Michezo

Carlo Ancelotti kutua Napoli muda wowote kurithi mikoba ya Maurizio Sarri

Aliyekuwa Meneja wa Chelsea, Real Madrid na Bayern Munich, Carlo Ancelotti ameanza mazungumzo na Rais wa klabu ya Napoli kwaajili ya kuwa kocha mpya wa timu hiyo.

Carlo Ancelotti yupo kwenye mazungumzo na rais wa klabu hiyo huko Italia ili kurithi mikoba iliyoachwa wazi na Maurizio Sarri ambaye alitangaza kuondoka siku ya Jumapili.

Napoli imemaliza nafasi ya pili ligi ya Serie A  msimu huu kwa kushinda jumla ya michezo 28 kati ya 38 

“Kwenye maisha kilakitu kinamwisho na nivema niishie hapa baada ya kuandika historia nzuri ,” amesema Sarri baada ya timu yake ya apoli kupata ushindi wa mabao 2 – 1 dhidi ya Crotone unaomfanya kumaliza msimu kwakuwa na jumla ya pointi 91 nyuma ya alama nne dhidi ya mabingwa wa Serie A timu ya Juventus.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents