Cassper Nyovest adai ‘Composure’ ya AKA ilimchoma!
Rapper Cassper Nyovest wa Afrika Kusini amezungumza kwa mara ya kwanza kuhusu maumivu aliyojisikia baada ya AKA kuachia single iliyomdiss.
Rappers hao wawili wamekuwa na uhasama kwa miezi sasa ikiwa pamoja na kutoa ngoma za kudisiana. Alianza AKA kwa kuachia ngoma yake Composure akimchana Cassper kuwa hana lolote.
https://www.youtube.com/watch?v=PhAYXZwnCek
Akiongea na waandishi wa habari jana jijini Johannesburg, Cassper alisema wimbo huu ulimshika pabaya kiasi cha kushindwa kunyamaza na hivyo kujibu kwa ngoma yake Dust2dust.
“I responded to AKA’s Composure because it got to me. It was personal for me, it got to me. As a man I had to respond,” alisema.
Aliongeza pia hata marafiki zake walimsihi asijibu lakini alishindwa kujizua.
https://youtu.be/cfkuUfFhy5w
“I walked away from having a gun to my head, from being slapped, but I could not walk away from Composure,” aliongeza.