Burudani
Cassper Nyovest ataja tarehe ya kuachia albamu yake mpya ‘Thuto’
Hatimaye, Cassper Nyovest ametaja siku ambayo ataiachia albamu yake mpya.
Albamu hiyo iliyopewa jina la ‘Thuto’ itaachiwa Mei 7 ya mwaka huu na itakuwa na nyimbo 16 ndani yake.
“#Thuto album track list. Model: Thuto Picture by: Thuto Release date: May 7th(Thuto’s Birthday) Preorder album now,” ameandika rapper huyo kwenye mtandao wake wa Instagram.
Kwenye albamu hiyo amewashirikisha wasanii kibao wakiwemo Goapele, Tshego, Tsepo Tshola, Nadia Nakai na Black Thought .