Burudani

Chambuso amtetea Aslay kwa WCB

Vita ya Diamond na Alikiba haijawahi kumuacha mtu salama.

Meneja wa Aslay, Chambuso amemtetea msanii wake huyo kuwa hajawahi kuwa na ukaribu na Alikiba. Hilo limekuja baada ya kusambaa maneno kuwa hitmaker huyo wa ‘Muhudumu’ ameingia kwenye mgogoro na WCB kutokana na ukaribu wake na Alikiba.

Akiongea Ijumaa hii katika kipindi cha FNL, Chambuso amesema, Aslay hajawahi kuwa karibu na Kiba na wala hakuwa na wimbo wowote ambao tayari wameurekodi kama inavyosemwa na baadhi ya watu. Ameongeza kuwa wala hakuna tatizo lolote kati ya Aslay na WCB.

Chambuso amepigilia msumari kwa kusema, nyimbo alizoachia Aslay ni kama zawadi hajaanza kufanya kazi rasmi ila baada ya kupita mwezi mtukufu wa Ramadhan wataanza kuachia nyimbo za msanii huyo rasmi.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents