Habari
Champions League: Chelsea watwaa ubingwa wa Ulaya
Chelsea wamefanikiwa kunjinyakulia kombe la Ligi ya Mabingwa Ulaya, kwa mara ya kwanza katika historia ya klabu hiyo, baada ya kuifunga Bayern Munich kwa penalti 4-3 kufuatia sare ya 1-1 ndani ya dakika 120 katika uwanja wa Allianz Arena jijini Munich, Ujerumani.
Ingawa kutakuwa na mengi ya kusemwa, pamoja na Bayern Munich kutawala mechi hiyo Chelsea wameibuka mabingwa na mpira ndivyo ulivyo.
Hongereni the Blues!