Afya

Chanjo ya Corona Afrika itachelewa sana

Karibu dozi milioni 900 zimepatikana hadi sasa kupitia mipango mbalimbali, ya kutosha karibu 30% ya watu bilioni 1.3 wa bara hili mwaka huu.


Kuhodhiwa na mataifa tajiri, upungufu wa ufadhili, kanuni na masharti vimepunguza mchakato wa kuzindua chanjo. “Ulimwengu uko ukingoni mwa kutofaulu kwa maadili na bei italipwa kwa maisha na maisha katika nchi masikini,” alionya mkuu wa WHO Dkt Tedros Ghebreyesus.


Wito wa usawa umekuwa ukiongezeka. Karibu dozi milioni 40 zimetolewa katika nchi zisizopungua 49, zenye kipato cha juu ikilinganishwa na dozi 25 tu zilizotolewa katika nchi moja tu ya kipato cha chini, kulingana na Dk Tedros. “Sio milioni 25, sio 25,000, ni 25 tu,” alisema, bila kusema ni nchi gani.


Kufikia sasa, hakuna chanjo kuu ambayo imeshatolewa barani Afrika, miezi miwili baada ya dozi ya kwanza kutolewa Ulaya.


Muungano wa mashirika na wanaharakati waliopewa jina la Umoja wa Chanjo ya Watu uligundua kuwa “mataifa tajiri yanayowakilisha asilimia 14 tu ya idadi ya watu ulimwenguni walikuwa wamenunua zaidi ya nusu (53%) ya chanjo zote.” Hiyo ilijumuisha chanjo zote za Moderna za 2021 na 96% ya uzalishaji unaotarajiwa wa Pfizer.


Canada iliongoza kwenye chati, kulingana na data na kampuni ya uchambuzi ya Airfinity, “ikiwa na dozi za kutosha za chanjo kwa kila raia wa Canada mara tano”. Mengi ya mahitaji hayo yanapaswa kutimizwa kabla nchi za kipato cha chini kufikiwa.


‘Usitafute faida kubwa’
Barani Afrika, hali hiyo inaamsha kumbukumbu za miaka ya 1990, wakati matibabu ya dawa ya kupunguza makali ya virusi vya ukimwi(ARV) ilipotengenezwa Marekani. Ingawa bara lilikuwa na idadi kubwa zaidi ya watu walioambukizwa VVU, ilichukua takriban miaka sita kabla ya matibabu ya kuokoa maisha kupatikana kwa Waafrika.


Watu milioni kumi na mbili walikufa barani Afrika kutokana na maradhi yanayohusiana na Ukimwi ndani ya muongo mmoja, pamoja na kupungua kwa vifo nchini Marekani, vkulingana na uchambuzi wa Vituo vya Afrika vya Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents