Michezo

Charles Mkwasa afanya mabadiliko kwenye kikosi cha Taifa Stars kinachotarajiwa kusafiri kwenda Nigeria

Kocha Mkuu wa timu ya Mpira wa Miguu Tanzania ‘Taifa Stars’, Charles Boniface Mkwasa, amefanya mabadiliko kwenye kikosi kinachotarajiwa kusafiri Jumatano Agosti 31, 2016 kwenda Nigeria kwa ajili ya mchezo wa mwisho wa kuwania kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2017) dhidi ya timu ya taifa ya nchi hiyo, Super Eagles.

Mkwasa1

Mabadiliko yaliyofanyika ni kwa kumchukua Kipa kinda wa JKT Ruvu, Said Kipao kuchukua nafasi ya Deogratius Munishi ambaye amefiwa na baba yake mzazi katika kifo kilichotokea jijini Dar es Salaam jana Agosti 28, 2016.

Licha ya mchezo huo wa Septemba 3, 2016 kuwa sehemu ya mchuano wa kuwania nafasi ya kucheza fainali hizo za AFCON 2017 huko Gabon, lakini utakuwa ni wa kukamilisha ratiba baada ya Misri kufuzu kutoka kundi G ambalo mbali ya Nigeria na Tanzania, pia ilikuwako Chad ambayo iliyojitoa katikati ya mashindano.

Wachezaji wanaounda kikosi hicho kwa sasa na kuanza kuingia kambini Hoteli ya Urban Rose jijini Dar es Salaam ni:

Makipa

Said Kipao – JKT Ruvu

Aishi Manula – Azam FC

Mabeki

Kelvin Yondani – Young Africans

Vicent Andrew – Young Africans

Mwinyi Haji – Young Africans

Mohamed Hussein – Simba SC

Shomari Kapombe – Azam FC

David Mwantika – Azam FC

Viungo

Himid Mao – Azam FC

Shiza Kichuya – Simba SC

Ibrahim Jeba – Mtibwa Sugar

Jonas Mkude – Simba SC

Muzamiru Yassin – Simba SC

Juma Mahadhi – Young Africans

Farid Mussa Tenerif ya Hispania

Washambuliaji

Simon Msuva – Young Africans

Jamal Mnyate – Simba SC

Ibrahim Ajib – Simba SC

John Bocco – Azam FC

Mbwana Samatta – CK Genk ya Ubelgiji

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents