Burudani

Cheche ya Ommy Dimpoz haikamatiki YouTube

Angalau kwa sasa Ommy Dimpoz anaweza akapumzika baada ya kuutua mzigo mzito wa lawama kutoka kwa mashabiki wake kuhusu kuchelewa kutoka kwa video ya wimbo wake mpya ‘Cheche’.

Hata hivyo hali hiyo inaweza ikawa ni neema kwa msanii huyo kutokana na mashabiki kutamani kuiona kwa muda mrefu. Video hiyo imefanikiwa kushika namba moja kwenye trending ya mtandao wa YouTube na kuzipiga chini video nyingine zilizouteka mtandao huo ikiwemo ‘Seduce Me’ ya Alikiba, ‘Zilipendwa’ ya WCB na ‘Unaibiwa’ ya Rayvanny.

Wakati huo huo, Cheche imefanikiwa kutazamwa mara 121,998 katika siku moja tangu ilipowekwa kwenye mtandao huo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents