Burudani

Chege apata ajali mbaya ya gari



Msanii wa Kigoma All Stars Chege Chigunda usiku wa jana amepata ajali mbaya ya gari maeneo ya Temeke jijini Dar es Salaam.
Taarifa za awali kuhusu ajali hiyo zimesema kuwa usiku huo Chege alikuwa ametokea jijini Nairobi.
Akiongea na mtangazaji wa Clouds FM, Diva kwenye kipindi cha Ala za Roho, Chege amesema usiku huo wa saa nne akiwa kwenye gari alikutana pikipiki katika mtaa mmoja wa maeneo ya Temeke ambaye alimgonga na yeye kupata ajali hiyo.
Chege amepata majeraha kadhaa lakini anaendelea vizuri licha ya gari lake kuharibika vibaya maeneo ya mbele.
Haikuweza kufahamika mara moja hali ya mtu huyo aliyekuwa na pikipiki.
Kupitia mahojiano hayo mafupi Chege amewatoa hofu mashabiki wake kuwa hali yake ni nzuri na yupo salama.
Kupitia website yake,Diamond amempa pole mwanamuziki mwenzie wa Kigoma All Stars kwa Nampa pole sana msanii Chege Chigunda kwa Ajali mbaya ya gari,Tumshukuru Mwenyezi Mungu kwa yote yaliyotokea……
Tufuatilia kwa karibu taarifa mpya zinazohusiana na ajali hiyo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents