Burudani
Chege atua South kushoot video na Justin Campos
Chege Chigunda amewasili nchini Afrika Kusini kwaajili ya maandalizi ya video yake mpya ya wimbo ‘Sweety Sweety’ aliyowashirikisha Runtown pamoja na Uhuru.
Akizungumza na Bongo5 akiwa nchini Afrika Kusini, Chege alisema kila kitu kinaenda sawa na muongozaji Justin campos kutoka kwa Gorilla Films ndio ataongoza video hiyo.
“Ndio tupo kwenye maandalizi ya video niliyomshirikisha, Runtown na Uhuru,” Chege ameiambia Bongo5. Hizi ni baadhi ya picha zao.