Burudani
Chege, Temba na Mataluma kuongeza nguvu Twanga
Bendi ya Twanga Pepeta imeongeza, wasanii Chegge, Mheshimiwa Temba na Mataluma kwa ajili ya kutoa burudani katika Tamasha la Twanga Pepeta linalotaraji kufanyika siku ya Jumapili tarehe 06-Novemba-2011 katika viwanja vya Leaders Club vilivyopo Kinondoni.
Tamasha hilo litakuwa ni kwa ajili ya Uzinduzi wa Albamu mpya ya Twanga Pepeta iitwayo Dunia Daraja na kusherehekea miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara.
Hawa ndiyo walioshirikiana kukamilisha wimbo wa Dunia daraja, akianzia kushoto wanataga kocha wa Dunia, Mwijuma muumini, Chaz Baba, Luiza Mbutu (Anayefuata jina limenipotea) wa mwisho ni Dogo Rama.