Michezo
Chelsea walistahili kupewa penati – Graham Poll (Picha)
Baada ya kocha wa Chelsea kulalamika kuwa walistahili kupewa penati kwenye mchezo wa jana dhidi ya Manchester United, aliyekuwa mwamuzi wa michezo ya ligi kuu ya soka nchini Uingereza, Graham Poll, amemkosoa mwamuzi aliyechezesha mchezo huo Philip Dowd kuwa hakutenda haki.
Poll, amesema ameufuatilia kwa umakini mchezo huo na kubaini Philip Dowd hakuitendea haki Chelsea kwa kuwanyima penati ya wazi ambayo kila mmoja alishuhudia tukio hilo.
Chelsea walikuwa wa kwanza kupata bao lililofungwa na Didier Drogba na baadaye Robin Van Parsie aliifungua Man United bao la kusawazisha katika dakika za majeruhi.