Burudani

Chris Brown aanza kujisogeza kwa Rihanna

Ukisema cha nini wenzako wanasema watakipata lini. Chris Brown ameanza kuwasha taa ya kijani kumfukuzia upya Rihanna.

Chris amemfollow Rihanna kwenye Instagram ikiwa ni muda mfupi baada ya taarifa za mrembo huyo kuachana na mpenzi wake, Hassan Jameel.

Hatua hiyo ya Chris imeonekana kama bado anamfukuzia mrembo huyo ambaye aliwahi kummiliki mwaka 2007 na walimwagana 2009.

Rihanna na Hassan ambaye ni tajiri wa Saudi Arabia wamekuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi tangu Juni mwkaa jana, ila imeripotiwa kuwa kwa sasa wameachana na Rihanna ndiye aliyevunja mahusiano hayo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents