Burudani
Chris Brown aongeza ulinzi nyumbani kwake kufuatia tukio la mwanamke aliyemkuta ndani!
Chris Brown anachukua hatua madhubuti kuhakikisha kuwa nyumba yake inakuwa salama zaidi baada ya hivi karibuni kumkuta mwanamke asiyemfahamu akiwa uchi ndani.
Kwa kuanzia kwa mujibu wa TMZ, Chris anafunga mfumo wa hali ya juu wa usalama ndani mwake.
Inavyoonekana ni kuwa mfumo wa zamani haukuwa imara kiasi cha kumfanya msichana huyo aitwaye Amira Ayeb kuvunja na kuingia ndani huku akifanya uharibifu.
Hata hivyo Brown hataki kumshitaki msichana huyo. Anadhani anahitaji kusaidiwa na sio kwenda jela.