Habari

Churchill show ya nchini Kenya yampoteza mcheshi wao mwingine

Kama wewe ni mpenzi wa buradani ya sanaa ya ucheshi Africa, basi Churchill show haiwezi kua kitu kigeni kwako. Ni kati ya ukumbi unaotumika kukuza vipaji vya wacheshi nchini Kenya na baadhi ya mastaa wakubwa kama Eric Omondi walipitia hapa kabla ya kuinuka na ulimwengu kuwakubali.

Show hii ambayo mwasisi wake ni mcheshi maarufu Daniel Ndambuki aka Churchill, jana tena ili mpoteza mmoja wao mcheshi maarufu Luthuoli Luthuoli.

Mcheshi huyu amekua akisumbuka na shida ya uvimbe kwenye ubongo, hali ambayo ilimfanya kupotea kuonekana kwenye jukwaa hili la sanaa kwa mda. Hadi jana usiku ndipo ilibainika kua nyota na mcheshi stadi kua hayupo tena. Bongo5 tunaungana na mashabiki wa Luthuoli kusema Mungu aipe faraja familia yake .

Imeandika na muandishi Changez Ndzai- Kenya

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents