Clinton na Trump wawabwaga wapinzani wao New York
Zaidi ya nusu ya kura zilizohesabiwa katika uchaguzi wa awali wa vyama katika kinyang’anyoro cha urais nchini Marekani katika mji wa New york, zinaonesha kwamba Donald Trump na Hillary Clinton wamepata ushindi mkubwa zaidi.
Hillary Clinton ambaye amemshinda mpinzani wake Bernie Sanders kwa ushindi mkubwa ameeleza katika hotuba yake kuwa ushindi wa chama chake cha Democratic umeweza kuwaunganisha zaidi wapinzani wake kuwa wamoja.
Hata hivyo New York inatajwa kuwa ngome nyingine ya Donald Trump,ambapo Cruz yeye hesabu za kura zake zimeonekana kugoma mapema kabisa katika chama chake cha Republican .
Wakati Hillary Clinton amemshinda mpinzani wake Bernie Sanders kwa ushindi mkubwa, amewaambia wapinzani wake kuwa kuna la ziada linalowafanya wawe wamoja zaidi ya kuwagawa.
Source: BBC