Burudani
Coca Cola yaandaa tamasha la bure la muziki Jumapili
Kampuni ya vinywaji baridi Coca cola Tanzania inatarajiwa kufanya tamasha la bure la burudani siku ya jumapili hii ya tarehe 17, katika viwanja vya Coco Beach, jijini Dar-es-Salaam.
Kwa mujibu wa waandaaji wa tamasha hilo ambao ni kampuni ya Coca Cola tamasha hilo litaanza kuanzia majira ya saa 6 mchana na halitakuwa na kiingilio. Burudani ambayo imethibitishwa ni pamoja na msanii Ommy Dimpoz, Joh Makini, Linnah, Wanaume TMK, Dj Zero na kundi la Swat Team.