Coutinho aigomea Liverpool, Manchester United, Arsenal, Barca na Juventus sokoni
Mshambuliaji wa Barcelona Philippe Coutinho, 27, amekataa uwezekano wa kurudi katika klabu ya Liverpool akidai kwamba yuko katika safari. (Sun)
Mshambuliaji wa Barcelona Philippe Coutinho, 27, amekataa uwezekano wa kurudi katika klabu ya Liverpool akidai kwamba yuko katika safari. (Sun)
Manchester United inachunguza hali ya kandarasi ya kinda wa Arsenal Bukayo Saka katika klabu hiyo. (Mail)
Mkufunzi wa Everton Carlo Ancelotti, 60, tayari ana matumaini kwamba kandarasi yake itaongezwa katika uwanja wa Goodison Park baada ya kutia saini kandarasi mnamo mwezi Disemba. (Mail)
Real Madrid imemuorodhesha mshambuliaji wa Everton Moise Kean, 19, katika rada yake ya kutaka kumsajili. (Teamtalk)
Borussia Dortmund itamruhusu mshambuliaji wa England Jadon Sancho, 19, kuondoka mwisho wa kandarsi yake na tayari wameanza kutafuta mchezaji atakayechukua nafasi yake. (Telegraph)
Manchester United ndio wanaopigiwa upatu kumsaini Sancho huku Chelsea ikitarajiwa kukamilisha uhaimsho wa kiungo mshambuliji wa Ajax Hakim Ziyech, 26.Chelsea inakaribia kukamilisha uhamisho wa dau la $38m
Liverpool itakabiliana na Real Madrid katika kuwania saini ya kiungo a kati wa Inter Milan Marcelo Brozovic, 27, mwisho wa msimu huu . (Star)
Mkufunzi wa klabu ya Chelsea Frank Lampard analenga kuwasajili wachezaji wane mwisho wa msimu huu utakaoigharimu Chelsesa £150m. (Metro)
Mkufunzi wa Juventus Maurizio Sarri amekiri kwamba Aaron Ramsey, 29, hajapata mambo kuwa rahisi wakati wa kipindi chake cha jeraha nchini Itali , na kuzua uvumi kwamba anapanga kurudi katika ligi ya England huku Arsenal, Manchester United, Liverpool na Chelsea zikihusishwa na uhamisho wake.. (Mirror)
Mshambuliaji wa Former Juventus na AC Milan Massimiliano Allegri ameripotiwa kufanya makubaliano na klabu ya England huku uvumi ukisema kwamba huenda akajiunga na Manchester United . (Corriere dello Sport, via Mail)
Arsenal inatarajiwa kuanzisha mazungumzo ya kandarasi mpya na Matteo Guendouzi, 20, ambayo yataongeza malipo ya mchezaji huyo. (Football.London)
Aston Villa ilishinda kumsaini Islam Slimani, 31, katika dirisha la uhamisho la mwezi Januari kwa kuwa mchezaji huyo wa Leicester hakutaka kucheza katika timu iiopo eneo la kushushwa daraja.. (Birmingham Mail)
Chelsea inpanga ya kumsaini upya Jeremie Boga, 23, kutoka klabu ya Sassuolo miaka miwili tu baada ya kumuuza winga huyo.. (Star)