Msanii CP ambaye anatamba na kibao chake 6 in the Morning’ hivi karibuni alionekana akipiga misele katika viwanja vya mawingu studio, jambo ambalo lilimfanya muandishi wa habari hizi atake kujua kulikoni.
Msanii CP ambaye anatamba na kibao chake 6 in the Morning’ hivi karibuni alionekana akipiga misele katika viwanja vya mawingu studio, jambo ambalo lilimfanya muandishi wa habari hizi atake kujua kulikoni.
Dah mtu wangu niko hapa kwa nia ya kuunda sumu mpya ambayo ni mapema sana kuizungumzia kwani mpaka sasa nadhani machizi wana hamu ya kusikia shughuli yangu mpya, na kama ilivyo kawaida yangu sina historia ya kukosea alisema Cp.
Aidha msanii huyu ameelezea kile anachotarajia kukifanya ni kutoka tofauti na ilivyozoeleka, kwani msela anatarajia kuja na staili ya crunk ambayo inafanywa na masupa staa kibao wa unyamwezini katika hali ya kuiboresha sanaa yangu nimeamua kufata matawi hayo-Cp.
nilichofanya ni kuchanganya prodaksheni kwani biti amenitengenezea mchizi wangu anayeitwa Lucci ambaye anafanyia shughuli zake nchini marekani, na sauti nimeingizia katika studio za mawingu kwa Papa Luvin chini ya produza Jay alisema.
Pwah’ ndio jina la ngoma hiyo ambayo iko katika mahadhi hayo ya crunk, dah kusema ukweli ngoma ni imesimama ile kinoma ukizingatia jamaa ni mmoja kati ya wasanii wenye staili ya tofauti na sauti yenye kuwavutia washabiki wa Muziki wa Bongo Fleva.
To listen to the track Pwaa press play – {mmp3}pwaa.mp3{/mmp3}
Source: Bongo5