Michezo
Cricket Tanzania yawaka.
Kundi la wachezaji wa Kriketi linalojulikana kama Caravan limeandaa mashindano ya kirafiki yanayotarajiwa kutimua vumbi Jumapili katika viwanja vya Tanganyika Packers Kawe jijini Dar es salaam.
Mkurungenzi wa kundi hilo,Vakakkiri Mohandas alisema, ‘Mwaka jana zilishiriki timu 16 na kombe kuchukuliwa na kambi iliyoandaa mashindano hayo. Mwaka huu kazi itakuwa ngumu zaidi na ushindani utakuwepo kwani zinatarajiwa kushiriki timu 21.’
Aliongeza kuwa, ‘Wachezaji 105 watakaoshiriki kwenye michuano hiyo ambayo fainali itachezwa desemba 12. Tumejiandaa vya kutosha kutwaa ubingwa huo.’