Michezo
Cristiano Ronaldo aifikia rekodi ya Raul, Real ikishinda 2-0
Mwanasoka Cristiano Ronaldo amefikia rekodi ya mabao ya Raul katika Ligi ya Mabingwa Ulaya, baada ya kuifungia mabao yote, Real Madrid ikishinda 2-0 ugenini dhidi ya Malmo FF dakika ya 29 na 90 Uwanja wa Swedbank mchezo wa Kundi A.
Ronaldo anakuwa amefikisha mabao 82 katika mechi za Ligi ya Mabingwa na mabao 501 jumla tangu aanze kucheza soka pamoja na kumfikia kwa mabao gwiji wa Real, Raul aliyekuwa anaongoza kuifungia mabao mengi klabu hiyo.