Michezo

Daktari wa Simba SC athibitisha Emmanuel Okwi yupo fiti

Daktari wa klabu ya Simba, Yassin Gembe amesema kuwa mshambuliaji wa timu hiyo raia wa Uganda, Emmanuel Okwi anaendelea vizuri kufuatia majeraha aliyopata kwenye mchezo uliyopita dhidi ya Mbao FC.

Gembe amesema kuwa Okwi anaendelea vizuri ukilinganisha na alivyokuwa hapo hawali na kunauwezekano mkubwa wa kuwepo katika mchezo ujao dhidi ya Stand United unaotarajiwa kupigwa siku ya Ijumaa.

Okwi anaendelea vizuri sana tofauti na jana, kwa hali aliyonayo pamoja na tiba ambazo tumeshampatia ni asilimia kubwa sana kwa yeye kuwepo kwenye mchezo unaofuata dhidi ya Stand United Ijumaa hii

Simba inaongoza katika msimamo wa ligi kuu soka Tanzania Bara kwa kuwa na jumla ya pointi 45 huku mshambuliaji wake huyo raia wa Uganda akiwa kinara wa mabao katika mbio za kuwania kiatu cha dhahabu kwa kujikusanyia jumla ya mabao 16 kibindo dhidi ya mchezaji wa Yanga SC Obrey Chirwa mwenye magoli 11 huku nafasi ya tatu ikishikiliwa na John Bocco wa Simba SC aliyo na goli zake 10.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents