Dar usafi bado ziro
Katika suala la wilaya mbali mbali kuanzisha mikakati ya kuliweka jiji safi la Dae es salaam katika hali ya usafi, kila siku linagonga mwamba kutokana na hali ya jiji kuzalishwa takataka nyingi huku zikikosa sehemu maalum za kuzihifadhi takataka hizo.
Miongoni mwa sehemu ambazo zimekuwa kero kutokana na uchafu kuwa mwingi kuanzia kwenye mitalo hadi maeneo mengine ya wazi ni Kariako, na ndiyo miongoni mwa sehemu zinazotembelewa na wageni wengi. sijui tunawaonyesha wageni nini kuhusiana na hali hiyo ya kuanika takataka mbele ya maduka makubwa ya wafanya biashara, wadogo wadogo na wakubwa.
Hii ni sehemu ambayo abilia mbalimba hugoja magari, na ndipo takataka zimekuja zikiweekwa papo hapo huku zikitoa harufu mbaya, wakati zikisubiri usafiri.
Kweli usafi kwetu tutaendelea kuusikia kwenye maredio na wala si vitendo, na hatiujifunzi mpaka magonjwa ya mlipuko yatokee kama vile kipindupindu