Burudani
David Moyes atimuliwa kama kocha wa Real Sociedad
David Moyes ametimuliwa kama kocha wa klabu ya Real Sociedad ya Hispania, mwaka mmoja baada ya kuinoa.
Kocha huyo mwenye miaka 52 aliyefanya timu yake imalize msimu uliopita wa ligi ya La Liga katika nafasi ya 12, alijiunga nayo November 2014.
Maelezo kutoka Sociedad yamedai kuwa imeamua kuusitisha mkataba wa Moyes. Kocha msaidizi, Billy McKinlay naye amefungashiwa virago.
Moyes alichukuliwa na Sociedad baada ya kutimuliwa kama kocha wa Manchester United April 2014.