Burudani

Davido aliahidi kunipa mil. 50 atembee na shemeji yangu – Atoboa siri mpiga picha maarufu nchini Nigeria

Mpiga picha wa kiume maarufu nchini Nigeria, ambaye anatumia jina la @iamtberry kwenye mitandao ya kijamii ameamua kuchafua hali ya hewa nchini humo baada ya kuonesha charts za yeye na Davido zikionesha mnyamwezi Davido akimshawishi amkowadie shemeji yake.

Berry kwenye posti zake aliibua maswali mengi ambapo watu wengi waliona kama ni kitendo cha kumharibia Davido mahusiano yake mapya, jambo ambalo lilimulazimu azifute posti hizo mtandaoni.

Berry aliandika kuwa mapema mwa mwezi Juni aliposti picha ya shemeji yake kwenye ukurasa wake wa Instagram na muda mfupi baadae Davido akaja DM akihitaji jina la shemeji yake ambalo anatumia mtandaoni (username).

Berry anasema alimdanganya Davido kuwa mrembo huyo hayupo kwenye mitandao ya kijamii na bado ni mwanafunzi na ni shemeji yake, ndipo Davido alipoanza kumshawishi kwa hela akiahidi kumpa Naira milioni 7 sawa na Ths milioni 51 lakini alimkatalia.

Aliongeza kuwa angewasafirisha wawili hao mpaka Nigeria kutoka Marekani ambako alikuwa anafanyia kazi kipindi hicho, lakini Berry anadai alikataa kwani asingeliweza kumuuza shemeji yake.

Hata hivyo, katika hali isiyokuwa ya kawaida Davido alimjia juu kwenye kisanduku cha maoni (Comments) kwenye Posti za Berry, akimwambia kuwa alitaka kufanya naye kazi na sio upuuzi ambao aliouandika.

Mpiga picha huyo, baada ya komenti ya Davido alimjibu kuwa ni utani na akaamua kufuta posti zote tatu alizoweka screenshots za charting zake na Davido.

Tayari mpiga picha huyo, kupitia ukurasa huo huo wa Instagram baada ya kufuta posti za kumchafua Davido, ameomba radhi na kutangaza kuwa kesho anaachia ngoma mpya, wengi wameitafsiri mchezo huo kuwa ni kiki. Pitia baadhi ya maoni ya wadau

mz_eddy@yougetjesus and he added you to his will abi….. bet you don’t even have a purpose in this life…not like he knows you exist…. be a fan and don’t forget it’s just music!!! He isn’t paying you!

sahmi_king@diorbecca I hope you know your brother is not worth davido’s time! It will be a waste of time to drop a sick comment here because David is just making your bro known honestly and he doesn’t really tag people to his insta story so I am very sure all this is bullshit his just trying to grow your bro’a followers..so y’all better stop playing with our heads.

davidoarmyss@diorbecca that’s enough..when all hell break lose on your brother which isn’t going to happen you can’t handle it…he already apologized and that’s it…#nofighting

noifsorbutsssCan someone explain to me what happened?

skellyjay1255Though I love davido die but I don’t understand why all this fights bro…anyway I like your job bruh…bigger you I pray and bro forget that thing you don blow for naija and now am learning something and I believe every disappointment is a blessing…I wish person go fit say make them insult me gan so I can blow hahaha…bravo bro if I grow I go like be like you ooooo…love your work die and God bless.

 

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents