Burudani
Davido asaini msanii mpya ndani ya lebo yake ya DMW
Davido ameendelea kutanua himaya ya lebo yake ya Davido Music Worldwide (DMW) kwa kumsaini msanii mpya.
Alhamisi hii muimbaji huyo amefanikiwa kumsaini msanii Peruzzi kupitia lebo yake hiyo.
Baada ya kufanikiwa kupata dili hilo, Peruzzi kupitia mtandao wake wa Instagram ameandika, “It’s called??? I FEEL BLESSED TO BE WELCOMED ON THIS PLATFORM… TIME TO LET THESE MUSIC HEAL THE WORLD!!!!! #TakeOver ✊✊✊ God Bless You @davidoofficial @kingpatrickgb @kolotainment WE MOVE!!!.”
Wasanii wengine ambao wanasimamiwa na lebo ya Davido ni pamoja na Yonda Music, Mayorkun, Dremo, Ichaba na mrembo Lola Rae.