Michezo
Davido ashindwa kuvumilia kipigo cha Barcelona kwa Real Madrid ‘nimepatwa na msongo wa mawazo’
Msanii wa muziki kutoka Nigeria, Davido ameamua kuweka wazi hisia katikati ya mchezo kati ya timu yake ya Real Madrid dhidi ya Barcelona.
Davido kunako kipindi cha pili dakika 85 ya mchezo wakati Barcelona wakiongoza kwa goli 4-1 ali-tweet na kuandika “Jamani napatwa na msongo wa mawazo Barcelona wanacheza sana“.
Omo Barca Dey para
— Davido (@davido) October 28, 2018
Davido ambaye ni shabiki wa kutupwa wa Real Madrid, alishawahi kueleza kuwa sababu kubwa ya kuishabikia Real Madrid ni kutokana na uwepo wa Cristiano Ronaldo.
Kwenye mchezo wa leo wa El Clasico, Barcelona wamechomoza na ushindi wa goli 5-1 dhidi ya Real Madrid.