Burudani

Davido athibitisha Chris Brown atakuwa mpambe wake siku ya harusi “Vuta picha Chris yuko pembeni yangu na vazi maalumu”

Davido athibitisha Chris Brown atakuwa mpambe wake siku ya harusi "Chris amekubali kuwa mpambe wangu hebu vuta picha Chris yuko pembeni yangu"

Msanii wa muziki kutoka nchini Nigeria David Adedeji Adeleke alimaarufu Davido, ambaye siku za nyuma alitioa taarifa kwamba atafunga ndoa na mchumba wake Chioma mwaka 2020.

Davido kupitia ukurasa wake wa Tweeter ametupa taarifa kwamba Chris Brown anaweza kuwa mpambe wake siku ya harusi yaani (Best man) kwenye siku yake hiyo kubwa na ya kihistoria. Kuanzia Kanisani hadi ukumbini bega kwa bega.

Maneno ya Davido yanasomeka hivi:-  “Chris amesema anataka kuwa mpambe wangu, hebu fikiria unamuona Chris kwenye vazi maalum la heshima.”

By Ally Juma.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents