Burudani

Dayna Nyange alikataa ofa ya madirector 3 waliotaka kushoot video ya ‘Komela’ bure

Hitmaker wa wimbo wa ‘Komela’ Dayna Nyange amedai kuwa kuna watayarishaji watatu walitaka kuufanyia wimbo wa Komela video lakini aliwakatalia.

dayna-nyange

Muimbaji huyo amekiambia kipindi cha Planet Bngo cha EA Radio kuwa sababu ya kufanya hivyo ni kutokana na baadhi ya vitu alivyovitaka havikukaa sawa.

“Nina directors zaidi ya watatu ambao wanataka kushoot video ya wimbo wa Komela lakini nilikataa kufanya nao kwa kuwa baadhi ya vitu vilikuwa havijakaa sawa,” amesema.

Dayna ameongeza kuwa video ya wimbo huo aliomshirikisha Bill Nas itatoka baada ya mwezi mmoja.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents