Habari
DC Malinyi na Mkurugenzi wake, Mussa Mnyeti watumbuliwa na Rais Magufuli
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Magufuli leo Septemba 17, 2019 ametengua uteuzi wa Mkuu wa Wilaya ya Malinyi, Majura Kasika na Mkurugenzi wa Wilaya hiyo, Mussa Mnyeti.
Utenguzi huo umekuja siku moja baada ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kuonesha kukerwa na viongozi hao kutokuwa na uhusiano mzuri, hivyo kuathiri utendaji kazi wao.