Michezo
De Gea asaini mkataba mpya Manchester United
David de Gea baada ya kuona ndoto zake za kuhamia klabu ya Real Madrid zimekwama baada ya siku ya mwisho ya uhamisho amemua kukubali tu ya ishe na sasa amesaini mkataba wa miaka minne Manchester United.
David de Gea akiwasili katika uwanja wa mazoezi wa Manchester United
Mlinda mlango, 24, alifanya mazungumzo baada ya uhamisho wake wa pauni milioni 29 kugonga mwamba kwenda Madrid.
Wakala wa De Gea ambaye alienda hadi uwanja wa mazoezi wa United Jorge Mendes, Siku ya Alhamisi kwa ajili ya mazungumzo zaidi na kocha Louis van Gaal na maafisa wa klabu. Waliungana na De Gea pamoja na wanafamilia yake.