Denzel Washington kushoot filamu nchini Nigeria
Muigizaji wa Hollywood, Denzel Washington anatarajiwa kuwasili nchini Nigeria wiki ijayo ili kushoot filamu mpya iitwayo Spider Basket.
Filamu hiyo imefadhiliwa na mfanyabiashara wa Nigeria Dennis Osadebe.
Uamuzi wa Osadebe kumchukua Denzel Washington kuigiza kwenye filamu hiyo pamoja na waigizaji wa Nigeria ni kumtaka muigizaji huyo ashuhudie vipaji vya uigizaji vilivyopo nchini humo.