Burudani
Destiny’s Child kurekodi album mpya, asema baba yake Beyoncé
Mathew Knowles amedai kuwa kundi la Destiny’s Child linaloongozwa na mwanae, Beyoncé – litarekodi album yake mpya na Michelle Williams tayari amethibitisha.
Baba yake Beyoncé aliyelisimamia kundi hilo amedai kuwa mipango inaendelea kwa wasichana hao, Michelle, mwanae na Kelly Rowland, kuingia studio na kurekodi album mpya.
Mathew aliliambia jarida la Heat kuwa alipokea email kutoka kwa Michelle aliyemwambia kuwa yupo tayari kuungana na wenzake kwaajili ya ujio mpya.
Mathew aliwahi pia kuwa meneja wa Beyoncé lakini aliachishwa kazi mwaka 2011.