Usiku wa Jumamosi ulikuwa mzuri kwa kundi la Destiny’s Child ambalo linasifika kwa hits nyingi pamoja na kuwatoa wanamuziki wake Beyonce na kelly Rowland.
Kuonekana kwa pamoja kwa kundi la Destiny’s Child, katika maonyesho ya picha ya ‘Wearable Art Gala’ yaliofanyika makumbusho ya ‘California Africa America’ mjini Los Angeles Marekani, kumeashiria huenda kundi hilo litarudi tena kwenye muziki pamoja,kama ambavyo awali ilisemakana.
Katika usiku huo Beyonce alionekana akiwa na mumewe Jay Z pamoja na mtoto wao Blue Ivy , wakiwa wenye furaha katika maonesho hayo yalioandaliwa na mama yake Beyonce Tina Lawson.
Hawa ni baadhi ya watu maarufu waliohudhuria;
Na Laila Sued