Michezo
Dhoruba ‘CIARA’ yasimamisha mechi ya Manchester City dhidi ya West Ham
Mchezo wa ligi kuu England baina ya Manchester City dhidi ya West Ham United umeghairishwa kufuatia kuwepo kwa hali mbaya ya hewa.
Mechi hiyo ambayo ilipaswa kupigwa leo siku ya Jumapili katika dimba la Etihad, umegharishwa kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya klabu ya Manchester City ambaye alikuwa mwenyeji wa mchezo.
Hali mbaya ya hewa inayokwenda sanjari na dhoruba Ciara (Storm Ciara) imepelekea kugharishwa kwa mechi hiyo na nyingine baadhi huko England zilizopangwa kuchezwa leo siku ya Jumapili.
Miongoni mwa mechi nyingine iliyoathiriwa na uwepo wa hali mbaya ya hewa ni ‘Derby’ ya north London baina ya Arsenal na Tottenham kwa upande wa ligi ya Wanawake Women’s Super. Hata hivyo wale waliyokata tiketi kwaajili ya kwenda kushuhudia mechi hizo, zitakuwa zipo hai kwa michezo inayofuata.