Burudani

Diamond afunguka kolabo yake na Rick Ross

Mkali wa muziki wa Bongo Flava, Diamond ameeleza mambo machache kuhusu kolabo yake na rapper wa Marekani, Rick Ross.

Muimbaji huyo ambaye kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake mpya ‘Hallelujah’ ameiambia Coconut Fm kuwa ngoma hiyo ni yake Rick Ross kashirikishwa tu.

“Ni wimbo ni wangu mpya nimemshirikisha Rick Ross, kusema wimbo unaitwaje hiyo bado” amesema Diamond.

Katika hatua nyingine amezungumzia ngoma yake ‘Hallelujah’ aliyowashirikisha Morgan Heritage kwa kusema ngoma hiyo alikuwa ameshafanya verse moja na chorus, hivyo walichofanya kundi hilo ni kutuma verse yao tu na mchezo ukawa umeisha.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents