BurudaniDiamond Platnumz
Diamond akata mzizi wa fitina
Baada ya bwebwe na maneno ya hapa na pale msanii Nasib Abdul ameamua kufunga kazi na kuachana na maneno ya kuzushiana kwa kumvisha pete ya uchumba laazizi wake Wema Sepetu katika ukumbi wa New Maisha Club wakati wa sherehe za kuzaliwa kwake.
Mwanamuziki huyo aliyatimiza hayo baada ya minong’ono ya hapa na pale kwamba anahitaji kumfanyia ‘Suprise’ aka Mshangao katika siku hyo, na watu kumtafsiri tofauti kwani kila mmoja aliongea lake, lakini mwisho wa siku aliamua kukata mzizi wa fitima kwa mdada huyo wa Bongo Movie na aliyekuwa miss Tanzania mwaka 2006. Ni hayo tu….