Burudani

Diamond amlilia Mzee Kikwete ‘tumekukumbuka, wasanii hatuna thamani wala umuhimu tena’

Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz ameamua kueleza hisia zake kupitia salamu za kumtakia kheri Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete.

Related image

Diamond kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika kuwa, kwa sasa Wasanii wa muziki wamem-miss sana Mzee Kikwete kwani uongozi wa sasa umewazuia hata kutumbuiza kwenye kampeni.

BONGO FLAVA GODFATHER…WE LOVE & MISSING YOU 😪😭😭😓😭. Vijana wako leo tumeambiwa hatuna tena umuhimu, hatutakiwi tena kwenye Kampeni. Hatuna tena thamani what can we say? sawa tunashukuru, ila tumeumia,“ameandika Diamond Platnumz.

Jana Oktoba 8 ilikuwa ni siku ya mfanano ya kuzaliwa kwa Dkt. Jakaya Kikwete ambapo alikuwa anaadhimisha miaka 67.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents