BurudaniUncategorized

Diamond amtolea uvivu Q-Boy Msafi, ‘Nikiamua nitamnyoosha’

Baada ya maneno mengi kuzunguzwa na QBoy Msafi kuhusu kupigwa chini na Lebo ya WCB, hatimae Diamond Platnumz amefunguka kwa mara ya kwanza akidai kuwa amemsikia kwenye mahojiano yake karibia yote akilalamika huku akitoa lawama kwa uongozi wa WCB kitu ambacho sio kizuri kwenye jamii.

Diamond Platnumz

Diamond Platnumz amesema Q-Boy Msafi alipewa adhabu ya kinidhamu na Uongozi wa WCB kama Ofisi zingine zilivyo akasimamishwa kwa wiki moja lakini yeye akaona kama ameonewa akaendelea kufanya vitu ambavyo vile vile alivyokuwa anakosea tena zaidi.

Unajua Ofisi kama Ofisi ina kanuni na taratibu zake na binadamu mnapokaa kwa pamoja haiwezekani mkawa perfect siku zote mimi mwenyewe sometimes nakosea Ofisi kama Ofisi inanipa adhabu zangu za kiofisi, inanikemea …aaahhh tulivyokaa na QBoy kwa takribani muda mrefu kuna vitu fulani fulani alikuwa anakosea lakini kama binadamu tunamuelewa na mimi nilikuwa mtu wa kwanza kumkingia kifua..

Kuna time akaja kuwa anapitiliza kwenye kukosea so kama ofisi ikiwa kuna watu wengine wanapewa adhabu wewe usipopewa adhabu inaonekana kama unapendelewa kwa hiyo nikampa adhabu ya kumsimamisha kama wiki mbili ili watu wengine wasione  labda kama yeye anapendelewa sasa yeye alivyopewa zile wiki mbili akaenda kufanya vitu vingine tofauti zaidi ndiyo suala limetokea hivyo,”alisema Diamond Platnumz huku akiendelea kusisitiza kuwa endapo ataamua kuchukua maamuzi kwa kivuli cha jina lake la Nassib basi atamnyoosha QBoy ndiyo maana akaamua kukaa kimya

“Kwahiyo suala hilo yeye akalichukulia tofauti na kuanza kuongea vitu vyote hivyo vingine tuu naamua kukaa kimya kwasababu mikiamua kusema sasa natumia Naseeb acha Diamond nikiamua kutumia Naseeb….ntamnyoosha“alisema Diamond Platnumz kwenye mahojiano yake na Clouds FM.

Hata hivyo Diamond Platnumz amesema kila binadamu anakosea na ili mtu aweze kujifunza kwani hakuna mtu aliyefanikiwa bila kukosea akitolea mfano kwa Kifesi ambaye nae alipewa adhabu kwa ya kusimamishwa kwa miezi sita lakini hakuwahi kuzungumza chochote nje ya WCB .

Diamond Platnumz jana aliachia video za nyimbo mbili mpya mmoja akiwa amemshirikisha Tiwa Savage kutoka Nigeria wimbo unaitwa ‘Fire’ na mwingine ‘I miss U’ akiwa peke yake unaweza ukazitazama video ya wimbo wake wa Fire hapa chini

By Godfrey Mgallah

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents