Burudani

Diamond anahusika kufanikisha kolabo ya Madee na Tekno

Msanii Madee amebainisha kuwa Diamond Platnumz anahusika kufanikisha kolabo yake na Tekno.

Madee amesema haikuwa ngumu sana kumpata muibaji huyo kutoka Nigeria na pia si yeye aliyeangaikia kolabo hiyo na hata pale Tekno alipoangalia kazi zake hakuwa na pingamiza kuhusu kufanya hiyo ngoma.

“Nilimuelezea tu Babu Tale pamoja na Diamond, bwana naweza kufanya kazi na Tekno?, wakasema inawezekana ngoja tumuambie nakumbuka alikuwa hapa hapa Dar es Salaam, wakamwambia akasema nipeni kama lisaa limoja ili nimuangalie huyu Madee,” ameiambia Bongo5 na kuongeza.

“Nadhani katika hilo lisaa limoja ndio akawa anamuangalia Madee ni nani, amefanya nini na ana impact gani baada hapo akawajibu its ok tunaweza kufanya lakini production nafanya mimi kwa sababu yeye ana studio,” amesema.

Ameongeza kuwa, “kwa hiyo akapiga ile biti akafanya vocal akaja tena Dar es Salaam kwenye mishe zake akatupatia ile biti pamoja na vocal nikaweka vocal zangu akapewa tena alipoona ipo ok,  ndio ikanyika mixing WCB,” amesema.

By Peter Akaro

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents