Burudani

Diamond ataja sababu ya kumshirikisha Young Killer kwenye wimbo wake mpya

Diamond amefunguka kwa mara ya kwanza sababu za kumshirikisha Young Killer katika wimbo wake mpya ambao bado haujatoka.

Ni mara nyingi hitmaker huyo wa Marry You, ameonekana kushindwa kuzizuia hisia zake za kumkubali Msodoki huku mara kadhaa akionekana kutumia mistari ya rapper huyo katika kuandika katika mitandao yake ya kijamii.

Akiongea na kipindi cha XXL cha Clouds FM Jumatatu hii, Diamond amesema,”Nilimuita Young Killer kuja studio, nikamwambia sijawahi kumshirikisha mtu katika muziki kipindi hiki na nikimshirikisha mtu ni wa WCB, kuna nyimbo yangu nataka nikushirikishe tufanye. Kwanza alipata shock kidogo, alipagawa kidogo”

“Nikamwambia usipagawe, hii nyimbo ukifanya verse mbovu nakufuta na hapa katika ofisi mimi ndio nimekupigania hili swala uingize verse kwa sababu kila mtu anashangaa kwanini Young Killer? Ile verse imeandikwa ndani ya siku hizi tatu, akanambia hii nyimbo angekuwa mtu mwingine ningeshamaliza. Katika intro ya kutafuta kuingilia alitafuta karibuni hata masaa sita, lakini mwisho wa siku amefanya verse kali sana sana, imeshaisha bado kushoot video ngoma itoke,” ameongeza.

Bosi huyo wa WCB amesisitiza, “Young Killer mtu ambaye masikini ya Mungu anajitahidi sana sana kufight na mtu ambaye anaandika, mimi napenda mtu anavyandika. Nikajua kwanza nikimchukua Young Killer, nitawaempower vijana wengine wengi wenye ndoto ya kufanya muziki kuona kwamba kumbe na sisi tunawezekana. Kwasababu wangejua Diamond angefanya ngoma labda na Fid Q na Joh, wao wanajua hizo ndio atafanya nao, lakini nimeonyesha kuwa yoyote ninaweza nikafanya naye nyimbo. Na Young Killer kiukweli anachokifanya ni kitu kikubwa na video tutashoot hapa hapa Tanzania na ngoma ni kali na yakinyamwezi.”

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents